KWA NINI YESU TU?
Kwa nini Yesu tu?
Wapo wengi waliozaliwa na wanawake lakin kuzaliwa kwa Yesu kulikuwa tofauti!
Wapo wengi waliotenda miujiza lakini miujiza ya Yesu ni aina yake na haina mfano wake, kumbuka miujiza ambayo Musa aliitenda, Eliya na Elisha!
Wapo wengi waliokufa lakin kifo cha Yesu ni cha tofauti ndo kiliturudishia mamlaka aliyokuwa ametulaghai shetani
Wapo wengi waliotundikwa msalabani lakini msalaba wa Yesu ndiyo nguvu ya waamini, ni ukombozi wa wanadamu, ni injili kamili!
Wapo wengi waliokufa na.kufufuka lakin ufufuo wa Yesu ni wa milele, na pia kwa ufufuo wake anatulisha kuwa miili yetu inapaswa kufufuliwa na naye!
Wapo wengi waliokuwa wana hekima lakini baada ya kufa kwao hekima yao inadumu kwa vitabu na makala mbalimbali lakn Yesu pekee ndiye hata mfupa haukuoza na bado anaishi na hekima yake ingali ktk kinywa chake!
Wapo manabii wengi sana waliopita lakin wengi wao bado hawakuwa wakamilifi km Yesu, mkumbuke nabii Isaya anasema kinywa changu ni kichafu n.k! Kumbula Musa, mkumbuke Daudi, Mkumbe Daniel anappsema nilipokuwa nikiungama dhambi yangu....! Mkumbe Ibrahim bado kuna mahali alidanganya, mkumbuke Paulo anappsema nakaza, mwendo, pia anasema naushulutisha mwili wangu ili nisiwe mtu wa kukataliwa! Ni Yesu pekee aliyesema ni nani anayenishuhudia kuwa nina dhambi!
Wapo walijaribiwa wakaanguka ktk dhambi, mfano, Adamu Daudi, Petro n.k ila ni Yesu pekee aliyeshinda kila majaribu ya shetani
Yapo mengi ya kujiuliza kuhusu Yesu but kumbuka kuwa aliyafanya hayo akiwa ni binadamu asilimia mia, akijaribu kutuonesha kuwa mtu aliyekombolewa kuwaje, mtu wa rohoni anapaswa kuwaje!
Yeye ndiye kielelezo halisi cha maisha ya Mkristo, tukishakombolewa tunakuwa viumbe wapya tuliozaliwa kwa jinsi ya rohoni, tunapokea tabia mpya za Kiungu huku tukiuvua utu wetu wa kale na kuvaa utu mpya wa Mungu ulioumbwa kwa ajili yetu!
Kumbuka alisema amwaminiye yeye atafanya makubwa kuliko aliyofanya Kristo! Bila shaka tunajua aliyoyafanya Kristo, ni mengi mno! Na anataka tufanye zaidi sisi tunaomwamini! Tujifunze kwake, tuisikie sauti yake, ninaamini anazangumza nasi siku zote akituelekeza ya kufanya ila masikio yetu ndiyo mazito, tumwombe Mungu atufungue kwa kuisikia sauti yake, je umepokea ujazo wa Roho Mtakatifu? Huyu ndiye mwalimu wetu, kiongozi wetu, msaidiz wetu, mfariji wetu na mpashaji wa yote yatolewayo na kinywa cha Kristo! Ndiye mfufuaji wa miili yetu iliyo ktk hatari ya kufa na ndiye alimfufua Kristo! Tuna nguvu hii ya Roho Mtakatifu ndani yetu km tumempokea!
Unapoendelea kutafakari kwa nini Yesu Kristo, hebu tafakari tena kwa nini naitwa Mkristo (yaani kwa nn usijiite mpagani)? na pia jiulize mpagani ni nani?
By Isaac Lwendela; Mkristo
No comments:
Post a Comment