UJANA WAKO UNADHAURIKA KWA LIPI?
1 Timotheo 4:12
Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi.
Katika nyakati za leo, vijana wamekuwa hawaaminiki katika kanisa wanaonekana wapenda usasa, wapenda dunia kuliko Mungu, wapapalikaji wa huduma na mengine.
Katika baishara wanaonekana matapeli, wapiga dili, wasioaminika, wanapenda njia za panya zaidi kufikia mafanikio na mengine mengi.
Katika kazi, makapuni na taasisi nyingi zimetokea kutokuwaamini vijana kwa sababu ya *wavivu, wachelewaji, wanapenda mapenzi kuliko kazi, wanapenda zaidi kuchati kuliko kazi yenyewe huku wakitegemea kupandishwa cheo, bonus na promotion.
Katika shule na vyuoni, vijana wajanya ni wale wazee wa mitoko, fashion za kila namna, misimu mikubwa kubwa, mapenzi kwa sana na starehe za kila namna, wakija mtaani mambo yanakuwa kinyume kabisa.
Vijana wapenda ajira kuliko kutengeneza ajira.
Vijana wenye kujiharibu kwa madawa ya kulevya, ngono, ukahaba, kuuza miili yao. Wasijue wapewa zamu moja tu duniani kuishi.
Vijana walio jaa matusi ya kila namna, lawama kwa serikali huku wakishinda vijiweni.
Kijana mwezangu utakuwa baba wa namna wa gani? Ewe binti utakuwa mama wa namna gani? Wa kuonesha maungu yako kwa watoto wako?
Je tutajenga taifa la namna gani? Nini hatima yako?
Kwa mambo hayo kwa nini ujana wetu usidharauriwe?
Kesho yako inaandaliwa na ujana wako wa leo. Unafanya sasa ni matunda ya kesho.
Kuwa mfano katika *usemi wako, kila ufanyalo, tabia, upendo, imani na usafi*
#Inuka ewe kijana mwenye nguvu.
#Ukajenge taifa na kuangaza
#Ukawe mfano wa kuigwa.
By Isaac Lwendela.
0768183433, 0679183438, 0783183433.
isaaclwendela@gmail.com.
No comments:
Post a Comment